Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Tuesday, August 6, 2013

Tendwa: Kwa heri, ila umedumaza Demokrasia


 
WAKATI aliyekuwa msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alikuwa akikabiliwa na Hamu ya kukifuta Chama cha Siasa cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye ulingo huo, hamu hiyo imedhihirishwa na usemi wa mkamia maji hayanywi na akinywa hutapika.
 
Kabla Tendwa hajakifuta Chadema, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo tarajio na makusudi ya Tendwa dhidi ya Chademea, yameyoyoma gizani.
 
Taarifa iliyotolewa Dar Es Salaam, Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.

 
Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria, akieelezwa na wadau wa Siasa na hasa wapinzani na Wapenda haki kuwa alikuwa kikwazo cha Demokrasia nchini.
Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, hivyo kuteuliwa kwake kumeelezwa na washiriki wana siasa kusipelekee yale aliyoyafanya Tendwa na kusababisha sintofahamu ya vurugu za Kidemokrasia.
 
Tumezoea kusikia mtu anapostaafu watu humzungumza kwa mazuri, lakini cha kusikitisha jamii kwa ujumla wake imekuwa na mtazamo hasi kutokana na wajibu wa Tendwa alipokuwa kwenye majukumu yake ya usajili wa vyama vya siasa.
 
Pengine niseme matatizo si changamoto aliyokuwa nayo Tendwa, sipendi yawepo kwa Jaji Mutungi, na tutakuwa na Imani hiyo kwa sababu kimsingi Mutungi wakati mwenzie akiwa katika wadhifa huo, alipata nafasi ya kusikia akilalamikiwa kwa mambo kadhaa, ayaepuke.
 
Ingawa muda wa Utumishi wa Tendwa ulikuwa umekwisha, lakini akapata bahati ya kuongezewa muda huo kwa msingi pengine alikuwa mtendaji mzuri wa kazi hivyo, utumishi ulikuwa bado unahitaji. Kilichodhaniwa na wengi sicho kilichojiri kwa wanasiasa na jamii.
 
Kiujumla nyakati hizi za mwishoni, Ofisi ya Msajili ikiongozwa na Tendwa ilikuwa na Kauli za Vitisho na Ubabe uliokuwa unakiuka Sheria kadhaa za Demokrasia ya Vyama Vingi, kiasi wadau wake walikuwa hawaamini iwapo ofisi hiyo ndiyo yenye watu wenye upeo wa Sheria.
 
Kwa kuwa wapenda Demokrasia na Maendeleo nchini wanamtarajia Jaji Mutungi atomize wajibu wake kwa kuzingatia haki, sheria na utawala bora, basi asije akapitia njia za Tendwa  
Ila anapaswa kuonesha kwa maneno na vitendo.
 
Aidha tunamtaka Jaji Mutungi aanze na kushughulikia matendo ya kiharamia ambayo yamekuwa yakifanywa kwenye chaguzi kubwa na ndogo, yaliyosababisha watu kupoteza maisha na ulemavu wa kudumu kwa wananchi na wanasiasa wote.
 
Hata hivyo Jaji pia anatakiwa kutoa Ushauri kwa Serikali na Jeshi la Polisi kuacha kutumia nguvu za ziada na Utawala Bora, juu ya uvunjifu wa sheria wa wazi uliokwisha fanywa na askari polisi dhidi ya vifo na kuumizwa kwa wandishi na wananchi, pasipo kosa lolote
 
Na Bryceson Mathias

No comments:

Post a Comment