Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Tuesday, August 13, 2013

KUTOKA FACEBOOK: Wilfred Rwakatare ameandika kutoka India anakopatiwa matibabu....

Habari waheshimiwa wananchi,poleni sana kwa majukumu ya kulijenga taifa.
Nikiwa ugenini India,napata mshituko na taarifa za kusikitisha kutoka huko nyumbani hasa juu ya rafiki yangu Sheikh Issa Ponda na wageni waliobahatika kuikanyaga ardhi ya Zanzibar.
kuna nini? manahodha wako wapi?
Salamu zangu za pole kwa swahiba wangu, ‘mjukuu wangu’ Sheikh Issa Ponda. namtakia uponyaji wa haraka na kila lenye kheri,naungana naye kwa sala. Pia niwape pole ndugu na watanzania wote waliozipokea habari hizi na kushika tama.
Nichukue fursa hii kukuhimiza wewe mheshimiwa,kutokuchoka kuliombea taifa letu la Tanzania, tunaziona dalili zote za kuipata Tanzania tuitakayo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment