Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Sunday, July 13, 2014

ZIARA ZA MBUNGE JOSEPH MBILINYI JIMBONI: HAPA NI ISYESYE - MBEYA

  •    PIA ALITUMIA FURSA HIYO KUZUNGUMZA NA WAKAZI WA ENEO HILO
 
 
 

 

 

Saturday, July 12, 2014

MBUNGE SUGU: AKABIDHI KAZI YA UJENZI WA DARAJA LA IYELA(MAKABURINI)

Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi "Sugu" amekabidhi kazi ya ujenzi wa daraja la Iyela(makaburini) kwa mkandarasi na tayari ujenzi huo umekwisha anza, daraja hilo kwa mujibu ya maelezo litajengwa likiwa limenyanyuliwa sana juu na litakuwa likipitisha magari yenye uzito hadi  tani 10, na  pichani ni kivuko ambacho kilianza kujengwa miaka zaidi ya 25 iliyopita na hakikukamilika.
Kwa wakazi wa Mbeya daraja hilo ni muhimu sababu ndiyo wanaitumia wananchi wa Mbeya kwa shughuli zao mbalimbali na haswa maziko sababu ndiyo eneo lina makaburi yanayotumiwa sana na wakazi wa Mbeya kwa maziko, na tatizo la daraja hilo lilipelekea watu kuzunguka umbali mrefu ili kufikia eneo hilo.

 

MBUNGE WA MBEYA MJINI - JOSEPH MBILINYI AHUDHURIA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI MBEYA MJINI KILICHOKETI KUJADILI TAARIFA MBALIMBALI ZA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELO KWA WANANCHI AMBACHO PIA NI KIKAO CHA MWISHO WA MWAKA.

 
 
 

Thursday, July 10, 2014

SUGU AJIBU MAPIGO YA CCM



BAADA ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), kumshambulia Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), ukimuita mpangaji katika jimbo hilo, amewajibu akisema kuwa wanaota ndoto za mchana.
Mbilinyi maarufu kama Sugu, alisema vijana hao hawazijui siasa za jimbo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa jana, Sugu, alisema vijana hao ndio wapangaji, na kwamba wasitarajie mteremko kwani yeyote atakayesimamishwa katika jimbo hilo kupitia CHADEMA ataibuka mshindi kutokana na wananchi wa Mbeya kuendelea kuwa na imani na chama hicho.
Alisema jimbo hilo alilikuta kama nyumba mbovu, akaamua kuinunua na baadaye akaivunja na kupandisha ghorofa, halafu aliyemuuzia anarudi na kudai nyumba ni ya kwake.
“Ndugu zangu, Jimbo la Mbeya ni sawa na Mkinga ama Mpemba aliyeenda Kariakoo, amenunua nyumba chakavu akaibomoa na kupandisha ghorofa zaidi ya tatu, halafu aliyeuza nyumba hiyo anaibuka na kusema hao watu ni wapangaji, si atakuwa anachekesha?” alihoji.
Aliongeza kuwa CCM hawana chao katika jimbo hilo kwa sababu sasa CHADEMA wanawaza kuchukua Halmashauri ya Jiji, na kwamba suala la ubunge haliwapi shida tena.
“Mikakati yetu ni kuchuka kata zote, lakini ili kuleta changamoto katika baraza ni vema tukawaachia kata kama nane ili kuleta changamoto katika Baraza la Madiwani,” alisema.
Kwa mujibu wa mbunge huyo, viongozi hao wa UVCCM wanafanya mikutano hiyo bila kuwa na taarifa kamili za jimbo hilo, kwamba ndio maana wamekuwa wakikurupuka na kutoa shutuma zisizo na ukweli wala utafiti wowote.
Alisema kuwa katika Kata ya Igawilo kulikuwa na mpango wa kujenga bwawa la samaki, lakini diwani wa kata hiyo kupitia CCM aliwashawishi viongozi wa serikali kugomea mradi huo kwa madai kuwa hitaji lao ni madawati.
Sugu alisema kuwa utafiti alioufanya alibaini mradi huo uligomewa na viongozi wa serikali za mitaa, ambao walipata shinikizo kutoka kwa diwani.
“Unajua watu wanaongea sana, ohoo aliahidi kuwa ataleta mradi wa samaki na mpaka sasa hakuna kitu, wananchi wengi hawajui, utekelezaji ulishaanza, lakini kutokana na ukiritimba wa baadhi ya wanasiasa pamoja na watumishi wa serikali wameukwamisha.
“Pale Uyole Nsalaga tulishachimba bwawa la samaki muda mrefu na nilishaongea na Mkurugenzi wa Jiji tukabaini kuwa maji yanayohitajika katika bili yake ni kama sh 200,000 kwa mwezi, lakini mpaka sasa hakuna kitu, wanazungusha tu bila kutoa sababu za msingi,” alisema Sugu.
Katika mikutano mingi ya CCM, wamekuwa wakijinadi kuwa jimbo hilo limepangishwa kwa muda kwa CHADEMA, hivyo uchaguzi ujao watalirejesha bila ugumu wowote.
Wakiongozwa na Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuwaapisha makamanda wa UVCCM kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Ruanda Nzovwe mwishoni mwa wiki, vijana hao wa CCM walisema kuwa Sugu ni mpangaji katika jimbo hilo, hivyo ajiandae kuondoka katika uchaguzi ujao.

Wednesday, July 9, 2014

SIKU SUGU ALIPOPANDISHA MIZUKA UWANJA WA SOKOINE

  • NI KATIKA MOJA YA MECHI YA MBEYA CITY FC

 



WAANDAMANA KUDAI KIDATO CHA TANO

  • WATINGA OFISI ZA MBUNGE JOSEPH MBILINYI NA MKUU WA MKOA 
  • WAANDISHI WA HABARI NAO WATINGA KUJUA HATIMA YA SAKATA HILI 
  • SUGU AONGEA NA WAZIRI NA KUHAKIKISHIWA SUALA HILI  LITATATULIWA MAPEMA
  • Wahitimu 39 wa kidato cha nne mwaka jana katika Shule ya Sekondari Karobe jijini hapa wakiwa na wazazi wao, jana waliandamana hadi ofisi za Mkuu wa Mkoa na pia wakaenda kwa Mbunge wa Mbeya Mjini ili kujua hatma yao baada Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kushindwa kuwapangia nafasi za kujiunga kidato cha tano licha ya kufanya vizuri katika mitihani yao.
    Wakizungumza wanafunzi na wazazi wao, walisema kuwa waliamua kufika ofisi za Mkuu wa Mkoa  pamoja na Mbunge wa Joseph Mbilinyi - Sugu  ili kujua hatima yake, baada ya kuona hawapewi majibu ya kuridhisha kutoka kwa viongozi wa chini yake.
     
    Walisema tangu wizara itangaze majina kwa ajili ya kujiunga kidato cha tano wiki mbili zilizopita, wameshangazwa kuona wanafunzi kutoka shule hiyo hawajapangiwa kwa ajili ya kuendelea na masomo katika ngazi hiyo, licha ya kuwa na ufaulu mzuri.
    Wanafunzi hao ambao wamepata alama za daraja la kwanza hadi tatu, hawajui hatima yao kutokana na wizara husika kushindwa kuwapangia shule kwa ajili ya kuendelea na masomo ya kidato cha tano.
    Nao wazazi ambao waliambatana na watoto wao hadi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (CHADEMA) kwa nia ya kutafuta suluhu ya suala hilo, walisema kuwa tangu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutangaza majina ya wanafunzi waliofaulu kwa ajili ya kidato cha tano na shule walizopangiwa, hakuna majina ya watoto wao na hatima ya watoto wao kwa sasa iko chini ya Mbunge wao huyo ili awasaidie kutatua hili suala.
     
    Mbunge huyo wa Mbeya mjini aliweza kuongea na Naibu Waziri wa Tamisemi - Elimu Kassim Majaliwa na Naibu Waziri huyo kumuhakikishia kuwa tatizo hilo lililotokana na Baraza la mitihani kutofikisha majina ya wanafunzi hao wizarani kwa wakati lakini limeshafika mezani kwake hivyo atahakikisha linatatatuliwa ndani ya siku chache zijazo.
    Mmoja wa wazazi hao, Lawrance Shimo, alisema baada ya kufuatilia kwa kina ikiwemo kuuliza uongozi wa shule, walibaini kuwa katika shule hiyo hakuna mwanafunzi hata mmoja aliyepangiwa shule kwa ajili ya kuendelea na kidato cha tano, licha ya kuwa na ufaulu wa alama nzuri.