Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Monday, June 15, 2015

MBUNGE JOSEPH O. MBILINYI ANASOMESHA KUPITIA MFUKO WA ELIMU

( muendelezo wa SUGU NA ELIMU - 2 )..... 

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph O. Mbilinyi "Sugu" anasomesha wanafunzi katika shule mbalimbali za sekondari, na hii ilitokana na baada ya kuanza kazi ya Ubunge moja ya changamoto aliyokumbana nayo ni wingi wa walezi na wanafunzi waliofika ofisini au waliomuona  kwa ajili ya kuomba msaada wa kusaidiwa ada na gharama nyingine za shule, ndipo ikapelekea aanzishe Mbeya Education Trust Fund (METF) au Taasisi ya Mfuko wa Elimu Mbeya.

Ambapo taasisi hii METF katika moja ya jukumu lake imeweza kusaidia wanafunzi wa sekondari  takribani 270 waliofaulu na hawakuwa na uwezo kutokana na  kuwa wanatoka kwenye familia zenye uwezo mdogo kiuchumi kwa kuwalipia ada na sare za shule pamoja na mahitaji mengine ya elimu pale inapobidi, na ilipoanza mwaka 2013 ilianza na watoto wa kidato cha 1 mpaka 4 (o'level) lakini sasa imeweza kusaidia mpaka wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 (A level).

Imetolewa na  OFISI YA MBUNGE MBEYA MJINI

(Chini ni picha mbalimbali za baadhi ya watoto wanaosomeshwa na Mfuko  huu wakiwa na Afisa wa METF)




No comments:

Post a Comment