Wakati wabunge watatu wa kambi ya upinzani, Mchungaji MSigwa, Tundu Lissu na Godbless Lema, wakitolewa nje ya bunge kwa kile kilichoelezwa na Naibu Spika, 'kuongea bila ruhusa', Mbunge wa Mbeya mjini kwa tiketi ya Chadema, Joseph Mbilinyi, a.k.a Mr II, amelilipua jeshi la Polisi nchini kwa kashfa. Akichangia mjadala kuhusu bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Mr. II alieleza kashfa za jeshi hilo alizoziona wakati akiwa mahabusu ya kituo kikuu cha Polisi, Mbeya. Mr. II alizitaja kashafa hizo kuwa:
Askari polisi 2 kuwekwa mahabusu moja na watuhumiwa wengine jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao
Wanafunzi wa chini ya umri wa miaka 18, wakiwa na sare zao za shule kuwekwa mahabusu na watu wazima
Wagonjwa 2 wa akili kuwekwa mahabusu moja na watuhumiwa wanganui na
Mwisho kubwa kuliko, mtuhumiwa wa kizungu kutokuwekwa mahabusu kama wengine, badala yake kutengewa ofisi na kufanywa ndiyo mahabusu yake, na zaidi ya hilo kupewa na 'house girl' wa kumuhudumia ambaye ni askari wa kike wa jeshilo. Kosa lake ni kukutwa na shehena kubwa ya pembe za ndovu!!
SOURCE: Global Publishers's News
Thursday, July 28, 2011
Mr. II alilipua Jeshi la Polisi Bungeni
Wednesday, June 29, 2011
Mbunge wa Mbeya Mjini akikagua mradi wa mabwawa ya samaki jijini Mbeya
Mh Joseph mbilinyi akisalimiana na wenyeji katika mradi huu wa ufugaji wa samaki
Hapa akipata maelekezo kutoka kwa wataalam wa ufugaji samaki ambao wali sema kwamba kwa bwawa lenye ukubwa huu ndani ya kipindi cha miezi mitatu na nusu bwawa hili lina uwezo wa kuzalisa tani saba mpaka tuni za samaki .
hatua ya kwanza ya ujazaji wa maji ya kuanzia yalipatikana katika mto ulio jirani na bwawa hili
ujazaji maji ukiendelea
chanzo cha maji ambacho kitakuwa kikitumika kujaza maji katika bwawa baada ya hatua ya kwanza kukamilika
Tuesday, June 28, 2011
Tahadhari na kauli za Pinda kuhusu Katiba Mpya
Tarehe 25 na 26 Juni 2011 Vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitangaza kwamba katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itazinduliwa tarehe 26 Aprili 2014 katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano.
Kufuatia ahadi hiyo ya Waziri Mkuu, baadhi ya wananchi wa Ubungo na vyombo mbalimbali vya habari mmetaka kupata kauli yangu kuhusu tamko husika. Naomba kuwasilisha kwenu maoni yangu yafuatayo:
Pamoja na kutambua kwamba hatimaye Serikali imetangaza muda rasmi wa ukomo wa kukamilika kwa mchakato husika bado ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inapaswa kupokelewa kwa tahadhari na anapaswa kutoa kauli ya kina bungeni itayoambatana na kuweka ratiba katika mipango, maazimio na sheria.
Hii ni kwa sababu katika Hotuba yake bungeni kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu na ofisi ya Bunge ya mwaka 2011/2012 Waziri Mkuu Pinda hakueleza tarehe hiyo badala yake alitoa tu kauli ya ujumla kwamba “Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba dhamira inatekelezwa ili nchi yetu iwe na katiba mpya kabla ya mwaka 2015”. Hivyo, ni muhimu ukomo huo wa Aprili 2014 kuwasilishwa rasmi bungeni kupitia kauli ya serikali au kupitia majumuisho ya hotuba ya Waziri Mkuu kabla ya mjadala wa muswada wa sheria na uzingatiwe katika mipango, maazimio na sheria.
Ikumbukwe kwamba tarehe 19 Disemba 2010 na 27 Disemba 2010 kupitia mikutano na wanahabari wakati nikieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi kuhusu mchakato wa katiba mpya na kutoa taarifa ya hoja husika nilieleza bayana kwamba kati ya mambo ambayo yanapaswa kupangwa na bunge ni pamoja na muda wa mchakato wa katiba mpya; suala ambalo lisingezingatiwa katika mchakato uliotangazwa awali kufanywa na serikali bila kuanzia bungeni.
Nilieleza wasiwasi wa wadau mbalimbali kuwa ukomo wa muda usipowekwa kwa mujibu wa sheria ama maazimio ya bunge, serikali inaweza kuchelewesha mchakato mzima kwa kutoa visingizio mbalimbali ili usikamilike mapema kuwezesha maandalizi ya kisheria na kitaasisi kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa kutumia katiba mpya.
Aidha umma unapaswa kuipokea ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa kupitia Semina Elekezi kwa wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala wa mikoa kwa tahadhari kwa kuwa imeambatana na kauli tata kuhusu mchakato mathalani serikali kutokuwa na uhakika kuhusu wakati ambapo muswada wa sheria ya mapitio ya sheria ya marekebisho ya katiba wa mwaka 2011 utawasilishwa bungeni.
Waziri Mkuu Pinda amenukuliwa akisema kwamba muswada huo utawasilishwa bungeni mwishoni mwa mkutano wa nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa au mwanzoni mwa mkutano wa tano wa bunge utakaofanyika Oktoba 2011; wakati katika mkutano wa tatu wa bunge Waziri Mkuu aliahidi kwamba muswada huo utarejeshwa katika mkutano wa nne wa bunge.
Ikumbukwe kwamba tarehe 30 Machi 2011 nilitoa tamko la kueleza kushtushwa na maudhui ya muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba wa mwaka 2011 (The Constitutional Review Act 2011) uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11 Machi 2011.
Nilieleza kwamba maudhui ya muswada huo yamedhihirisha tahadhari niliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya; matokeo yake ni muswada huo uliowasilishwa kwa hati ya dharura kuondolewa katika ratiba ya kupitishwa katika mkutano wa tatu wa bunge kutokana na shinikizo la wadau mbalimbali. Hivyo, Waziri Mkuu Pinda anapaswa kutoa kauli bungeni kueleza bayana iwapo hati ya dharura ya muswada huo ilifutwa basi muswada husika uwasilishwe kwa kufuata taratibu za kawaida kwa mujibu wa kanuni za bunge.
Pia, umma unapaswa kuipokea kwa tahadhari ahadi hiyo ya Waziri Mkuu kwa kuwa imeambatana na kutolewa kwa maelekezo kwa wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala kuhusu maudhui ya mchakato wa katiba na kipi kinakusudiwa kufanywa na serikali wakati ambapo bado sheria haijapitishwa na bunge.
Maelekezo hayo ya Waziri Mkuu Pinda yanadhihirisha kwamba tayari serikali imeshachukua msimamo kuhusu mchakato utakaotumiwa kuandika katiba mpya hiyo; hali inayoashiria kuwa serikali ina dhamira ya kulitumia bunge kama muhuri (rubber stamp) ya kupitisha mchakato ambao tayari ulishapitishwa ndani ya serikali na maelekezo ya utekelezaji kuanza kutolewa kwa watendaji wa serikali ngazi ya chini kabla ya sheria kupitishwa.
Ikumbukwe kwamba tarehe 30 Machi 2011 nilitahadharisha kwamba muswada uliowasilishwa bungeni umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na Rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali na yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na bunge kupitia muswada huo; mchakato ambao Waziri Mkuu Pinda ameurejea katika hotuba yake.
Kadhalika umma unapaswa kuipokea ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Pinda kwa tahadhari kubwa kwa kuwa imeambatana na maelekezo ya kuwataka wakuu wa mikoa na wilaya wawe mstari wa mbele kuongoza mchakato huo wakati inaeleweka wazi kwamba wadau mbalimbali wamelalamikia mamlaka waliyopewa watendaji wa serikali katika mikutano ya kukusanya maoni kuhusu katiba kwa mujibu wa muswada uliowasilishwa awali ambao wananchi walitaka vifungu husika vibadilishwe.
Ikumbukwe kwamba watendaji hao wamelalamikiwa kwa miaka kadhaa kutumia madaraka yao vibaya ikiwemo kudhibiti uhuru wa wananchi katika kutoa maoni kwenye tume mbalimbali ambazo zimewahi kuundwa na serikali nyakati za nyuma kwa masuala mbalimbali ikiwemo yanayohusiana na marekebisho ya katiba. Aidha kati ya mambo ambayo wananchi wameanza kuyatolea maoni kwenye maudhui ya katiba ni pamoja na kutaka kufutwa au kupunguzwa mamlaka ya wakuu wa mikoa na wilaya; hivyo kitendo cha kuwaweka mstari wa mbele katika mchakato ni dalili za serikali kutokuwa na dhamira ya kweli ya kutaka mabadiliko ya katiba.
Katika muktadha huo; na kwa kuwa serikali ilishawasilisha awali muswada wa katiba natoa mwito kwa Spika na Ofisi ya Bunge kuhakikisha kwamba bunge linachukua nafasi yake kuanzia hatua za msingi kuhakikisha suala hili la mchakato wa katiba mpya lipata uhalali wa umma kwa kurejea ibara 8 ambayo inatamka kwamba madaraka na mamlaka ni umma serikali inafanya kazi kwa niaba na Bunge ndicho chombo kikuu cha kusimamia wajibu huo kwa kutokana na mamlaka ya kikatiba yaliyopo kwenye ibara ya 63(2) na (3) yanayohusu kutunga sheria na ibara ya 98 inayohusika na mabadiliko ya katiba.
Hivyo, badala ya kusubiri mpaka mwishoni mwa mkutano huu wa bunge tarehe 29 mpaka 30 Agosti 2011 ndipo wabunge wapewe tena muswada wa mabadiliko ya katiba pamoja na marekebisho yake yaliyofanyika ikiwemo tafsiri katika lugha ya Kiswahili; utaratibu wa kikanuni ufanyike kuhakikisha taarifa ya serikali inatolewa mapema pamoja na muswada huo nyeti.
Kwa upande mwingine umma unapaswa kuzipokea kwa tahadhari kauli za Waziri Mkuu Pinda kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa kurejea msimamo wa wake wa awali kuhusu mabadiliko ya katiba alioutoa wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari tarehe 17 Disemba 2010 ulikuwa na kumshauri Rais aunde jopo shirikishi ili kuratibu na kusimamia mchakato husika.
Izingatiwe kuwa tarehe 9 Februari 2011 nilitoa tamko la kupokea kwa tahadhari uamuzi wa Serikali kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kubadili misimamo ya awali kuhusu mchakato wa katiba mpya na kuamua kukubaliana na mwito wa kutaka mchakato husika uanzie bungeni kupitia kutungwa kwa sheria ya bunge ya kuratibu na kusimamia mchakato husika kwa kuwa maneno ya kauli zilizotolewa hayaambatani na vitendo vya dhati vya kuweka mchakato mzuri wa katiba mpya.
Uthibitisho wa mwelekeo huo ni kwamba Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano (2011/2012-2015/2016) uliotiwa saini na Rais Kikwete tarehe 7 Juni 2011 haukuweka kipaumbele haja ya katiba mpya kwenye eneo la utawala bora na utawala wa sheria. Aidha, bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 haikuweka bayana na kwa kiwango cha kutosha rasilimali kwa ajili ya mchakato wa katiba mpya suala ambalo pamoja na maelezo ya Waziri wa Fedha wakati wa kuhitimisha hoja bado serikali ina wajibu wa kulitolea ufafanuzi wa kina katika mkutano wa Bunge unaoendelea.
kwa hisani ya
John Mnyika (Mb)
Kufuatia ahadi hiyo ya Waziri Mkuu, baadhi ya wananchi wa Ubungo na vyombo mbalimbali vya habari mmetaka kupata kauli yangu kuhusu tamko husika. Naomba kuwasilisha kwenu maoni yangu yafuatayo:
Pamoja na kutambua kwamba hatimaye Serikali imetangaza muda rasmi wa ukomo wa kukamilika kwa mchakato husika bado ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inapaswa kupokelewa kwa tahadhari na anapaswa kutoa kauli ya kina bungeni itayoambatana na kuweka ratiba katika mipango, maazimio na sheria.
Hii ni kwa sababu katika Hotuba yake bungeni kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu na ofisi ya Bunge ya mwaka 2011/2012 Waziri Mkuu Pinda hakueleza tarehe hiyo badala yake alitoa tu kauli ya ujumla kwamba “Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba dhamira inatekelezwa ili nchi yetu iwe na katiba mpya kabla ya mwaka 2015”. Hivyo, ni muhimu ukomo huo wa Aprili 2014 kuwasilishwa rasmi bungeni kupitia kauli ya serikali au kupitia majumuisho ya hotuba ya Waziri Mkuu kabla ya mjadala wa muswada wa sheria na uzingatiwe katika mipango, maazimio na sheria.
Ikumbukwe kwamba tarehe 19 Disemba 2010 na 27 Disemba 2010 kupitia mikutano na wanahabari wakati nikieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi kuhusu mchakato wa katiba mpya na kutoa taarifa ya hoja husika nilieleza bayana kwamba kati ya mambo ambayo yanapaswa kupangwa na bunge ni pamoja na muda wa mchakato wa katiba mpya; suala ambalo lisingezingatiwa katika mchakato uliotangazwa awali kufanywa na serikali bila kuanzia bungeni.
Nilieleza wasiwasi wa wadau mbalimbali kuwa ukomo wa muda usipowekwa kwa mujibu wa sheria ama maazimio ya bunge, serikali inaweza kuchelewesha mchakato mzima kwa kutoa visingizio mbalimbali ili usikamilike mapema kuwezesha maandalizi ya kisheria na kitaasisi kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa kutumia katiba mpya.
Aidha umma unapaswa kuipokea ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa kupitia Semina Elekezi kwa wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala wa mikoa kwa tahadhari kwa kuwa imeambatana na kauli tata kuhusu mchakato mathalani serikali kutokuwa na uhakika kuhusu wakati ambapo muswada wa sheria ya mapitio ya sheria ya marekebisho ya katiba wa mwaka 2011 utawasilishwa bungeni.
Waziri Mkuu Pinda amenukuliwa akisema kwamba muswada huo utawasilishwa bungeni mwishoni mwa mkutano wa nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa au mwanzoni mwa mkutano wa tano wa bunge utakaofanyika Oktoba 2011; wakati katika mkutano wa tatu wa bunge Waziri Mkuu aliahidi kwamba muswada huo utarejeshwa katika mkutano wa nne wa bunge.
Ikumbukwe kwamba tarehe 30 Machi 2011 nilitoa tamko la kueleza kushtushwa na maudhui ya muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba wa mwaka 2011 (The Constitutional Review Act 2011) uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11 Machi 2011.
Nilieleza kwamba maudhui ya muswada huo yamedhihirisha tahadhari niliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya; matokeo yake ni muswada huo uliowasilishwa kwa hati ya dharura kuondolewa katika ratiba ya kupitishwa katika mkutano wa tatu wa bunge kutokana na shinikizo la wadau mbalimbali. Hivyo, Waziri Mkuu Pinda anapaswa kutoa kauli bungeni kueleza bayana iwapo hati ya dharura ya muswada huo ilifutwa basi muswada husika uwasilishwe kwa kufuata taratibu za kawaida kwa mujibu wa kanuni za bunge.
Pia, umma unapaswa kuipokea kwa tahadhari ahadi hiyo ya Waziri Mkuu kwa kuwa imeambatana na kutolewa kwa maelekezo kwa wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala kuhusu maudhui ya mchakato wa katiba na kipi kinakusudiwa kufanywa na serikali wakati ambapo bado sheria haijapitishwa na bunge.
Maelekezo hayo ya Waziri Mkuu Pinda yanadhihirisha kwamba tayari serikali imeshachukua msimamo kuhusu mchakato utakaotumiwa kuandika katiba mpya hiyo; hali inayoashiria kuwa serikali ina dhamira ya kulitumia bunge kama muhuri (rubber stamp) ya kupitisha mchakato ambao tayari ulishapitishwa ndani ya serikali na maelekezo ya utekelezaji kuanza kutolewa kwa watendaji wa serikali ngazi ya chini kabla ya sheria kupitishwa.
Ikumbukwe kwamba tarehe 30 Machi 2011 nilitahadharisha kwamba muswada uliowasilishwa bungeni umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na Rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali na yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na bunge kupitia muswada huo; mchakato ambao Waziri Mkuu Pinda ameurejea katika hotuba yake.
Kadhalika umma unapaswa kuipokea ahadi hiyo ya Waziri Mkuu Pinda kwa tahadhari kubwa kwa kuwa imeambatana na maelekezo ya kuwataka wakuu wa mikoa na wilaya wawe mstari wa mbele kuongoza mchakato huo wakati inaeleweka wazi kwamba wadau mbalimbali wamelalamikia mamlaka waliyopewa watendaji wa serikali katika mikutano ya kukusanya maoni kuhusu katiba kwa mujibu wa muswada uliowasilishwa awali ambao wananchi walitaka vifungu husika vibadilishwe.
Ikumbukwe kwamba watendaji hao wamelalamikiwa kwa miaka kadhaa kutumia madaraka yao vibaya ikiwemo kudhibiti uhuru wa wananchi katika kutoa maoni kwenye tume mbalimbali ambazo zimewahi kuundwa na serikali nyakati za nyuma kwa masuala mbalimbali ikiwemo yanayohusiana na marekebisho ya katiba. Aidha kati ya mambo ambayo wananchi wameanza kuyatolea maoni kwenye maudhui ya katiba ni pamoja na kutaka kufutwa au kupunguzwa mamlaka ya wakuu wa mikoa na wilaya; hivyo kitendo cha kuwaweka mstari wa mbele katika mchakato ni dalili za serikali kutokuwa na dhamira ya kweli ya kutaka mabadiliko ya katiba.
Katika muktadha huo; na kwa kuwa serikali ilishawasilisha awali muswada wa katiba natoa mwito kwa Spika na Ofisi ya Bunge kuhakikisha kwamba bunge linachukua nafasi yake kuanzia hatua za msingi kuhakikisha suala hili la mchakato wa katiba mpya lipata uhalali wa umma kwa kurejea ibara 8 ambayo inatamka kwamba madaraka na mamlaka ni umma serikali inafanya kazi kwa niaba na Bunge ndicho chombo kikuu cha kusimamia wajibu huo kwa kutokana na mamlaka ya kikatiba yaliyopo kwenye ibara ya 63(2) na (3) yanayohusu kutunga sheria na ibara ya 98 inayohusika na mabadiliko ya katiba.
Hivyo, badala ya kusubiri mpaka mwishoni mwa mkutano huu wa bunge tarehe 29 mpaka 30 Agosti 2011 ndipo wabunge wapewe tena muswada wa mabadiliko ya katiba pamoja na marekebisho yake yaliyofanyika ikiwemo tafsiri katika lugha ya Kiswahili; utaratibu wa kikanuni ufanyike kuhakikisha taarifa ya serikali inatolewa mapema pamoja na muswada huo nyeti.
Kwa upande mwingine umma unapaswa kuzipokea kwa tahadhari kauli za Waziri Mkuu Pinda kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa kurejea msimamo wa wake wa awali kuhusu mabadiliko ya katiba alioutoa wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari tarehe 17 Disemba 2010 ulikuwa na kumshauri Rais aunde jopo shirikishi ili kuratibu na kusimamia mchakato husika.
Izingatiwe kuwa tarehe 9 Februari 2011 nilitoa tamko la kupokea kwa tahadhari uamuzi wa Serikali kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kubadili misimamo ya awali kuhusu mchakato wa katiba mpya na kuamua kukubaliana na mwito wa kutaka mchakato husika uanzie bungeni kupitia kutungwa kwa sheria ya bunge ya kuratibu na kusimamia mchakato husika kwa kuwa maneno ya kauli zilizotolewa hayaambatani na vitendo vya dhati vya kuweka mchakato mzuri wa katiba mpya.
Uthibitisho wa mwelekeo huo ni kwamba Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano (2011/2012-2015/2016) uliotiwa saini na Rais Kikwete tarehe 7 Juni 2011 haukuweka kipaumbele haja ya katiba mpya kwenye eneo la utawala bora na utawala wa sheria. Aidha, bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 haikuweka bayana na kwa kiwango cha kutosha rasilimali kwa ajili ya mchakato wa katiba mpya suala ambalo pamoja na maelezo ya Waziri wa Fedha wakati wa kuhitimisha hoja bado serikali ina wajibu wa kulitolea ufafanuzi wa kina katika mkutano wa Bunge unaoendelea.
kwa hisani ya
John Mnyika (Mb)
Saturday, June 18, 2011
Wabunge, waziri watunishiana misuli
- Friday, May 27, 2011, 5:03
- Habari kuu, Mtanzania
* Ni Kabaka, Jenista Mhagama, Mbilinyi (Sugu)
* Wavutana katika kutembelea kiwanda
* Kiwandani wabunge washuhudia ‘madudu’
* Wafanyakazi wanalazimishwa kuvaa kaptura
* Wabunge watokwa machozi kwa waliyoyaona
Na Arodia Peter
Dar es Salaam

WAZIRI wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Gaudensia Kabaka jana alivutana vikali na wabunge wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii waliokuwa wanataka kutembelea Kiwanda cha Vyombo vya Nyumbani cha Jambo Plastiki kilichoko Dar es Salaam.
Wakati wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa wamekwisha kujiandaa kwenda katika kiwanda hicho jana, ghafla Waziri Kabaka aliwaeleza kuwa ziara hiyo imeahirishwa hadi wakati mwingine.
Kabaka alitoa sababu za kutaka kuahirisha ziara hiyo kuwa ni mgogoro wa wafanyakazi na mwajiri kiwandani hapo ambao upo mahakamani hivyo ziara hiyo itakuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Baada ya kutolewa taarifa hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jenista Mhagama alikuja juu na kumweleza Kabaka kuwa kamwe kamati yake haiwezi kuahirisha ziara hiyo bila kutolewa sababu za kuridhisha. Alisema kitendo alichokifanya Waziri kinadhalilisha kamati yake.
“Mheshimiwa Waziri kitendo ulichokifanya unaingiza mgogoro mkubwa katika kamati ya Bunge… kwa mazingira ya sasa Watanzania hawana mahali popote pa kutolea shida zao zaidi ya bunge na hii inadhihirika wazi wataalamu wako hawakukushauri vizuri,” alisema Mbunge huyo wa Peramiho kwa tiketi ya CCM na kuongeza:
“Basi kama ni hivyo, Mheshimiwa Waziri mimi nakupisha uwe mwenyekiti wa kamati ya Bunge maana naona hutaki kutuelewa.”
Kuona hivyo, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alikwenda mbali zaidi kwa kusema kwa uzoefu uliopo nchini unaonyesha kuwa ziara hiyo tayari imekwicha kuchakachuliwa na wahusika kwa manufaa wanayoyajua wao.
Alisisitiza kwamba kama ziara itaahirishwa basi yeye hatakuwamo kwenye orodha hiyo.
Naye Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) alisema kama kamati haitaki kwenda kwenye kiwanda hicho yeye atapanga ziara yake kama mbunge wa Chadema na kwenda kusikiliza na kukagua mazingira kiwandani hapo.
Asumpta Nshunju (CCM) ambaye ni Mbunge wa Nkenge, alisema kuna dalili za wazi watu wamepokea chochote kutoka kwa mwekezaji ndiyo maana kamati imepigwa ‘stop’ dakika za mwisho.
Akimsaidia waziri wake, Ofisa Kazi Mfawidhi wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Josephat Rugakingira aliwaambia wabunge kwamba haingekuwa vizuri kutembelea kiwanda hicho wakati mgogoro kati ya menejimenti na wafanyakazi bado uko Baraza la Usuluhishi wa Migogogro (CMA) ikiwa imefunguliwa kesi namba DMA/DSM/ILALA/ 2009.
Hata hivyo baada ya mvutano mkali hatimaye Waziri Kabaka alikubaliana na wabunge na kuamua kufanya ziara kiwandani hapo wakati huo ikiwa saa 7.00 mchana.
Kiwandani
Wabunge walipofika kiwandani walipangua ratiba iliyokuwa imeandaliwa iliyotaka wafanyakazi na menejimenti kukutana na kamati ya Bunge kwa pamoja.
Kamati ya Bunge iliamua kukutana na wafanyakazi pekee, kikao kilichodumu kwa zaidi ya saa moja. Waandishi wa habari wa menejimenti hawakuruhusiwa katika kikao hicho.
Baada ya kumalizika kikao hicho, wabunge walitoka nje wakiwa wanafuta machozi na baadhi yao walisema waliingiwa na simanzi kubwa kutokana na mambo mazito waliyoelezwa katika kikao hicho.
Hata hivyo, ilibainika kuwa katika kikao hicho ambacho Waziri pia alishiriki, kesi iliyokuwa inasemwa kuwa ipo mahakamani haikuwa kweli kwa vile ilikwisha kutolewa uamuzi tangu mwaka 2009.
“Hii kama siyo rushwa ni nini, ndiyo maana walitaka kutuchakachua tusije hapa kwa maslahi yao, hii ni aibu. Wataalamu wa Wizara ndiyo wanaotufanya sisi wabunge wa CCM tuonekane hatuna thamani mbele ya umma… kumbe ni watu wachache waliojiwekea mtandao wa rushwa kwa njia wanazozijua wao,” alisema mmoja wa wabunge kwa sharti la kutotajwa jina.
Waziri Kabaka akiri, aiomba radhi kamati
Baadaye Waziri Kabaka aliomba radhi kwa Kamati ya Bunge kutokana na hali iliyojitokeza awali. Alisema yeye hakujua kama alichoambiwa na wataalamu wa Wizara yake kilikuwa ni uongo na uzushi.
“Mheshimiwa mwenyekiti naomba radhi kwa yaliyotokea, nakiri nilidanganywa sasa nimejifunza kutoka kwenu,” alisema Kabaka kwa sauti ya upole.
Alipoulizwa na waandishi wa habari ni hatua gani atawachukulia wataalamu waliomdang’anya, alisema:
“Niachieni nitashughulika nao, tutaongea na wenzangu tuone ni kwa nini wamefanya hivyo”.
Wafanyakazi wanalazimishwa kuvaa kaptura
Kiwandani hapo wabunge walishuhudia wafanyakazi wakike na kiume wakiwa wamevaa kaptura na fulana ikiwa ndiyo sare za kiwanda hicho.
Wakizungumzia hali hiyo baadhi ya wafanyakazi walisema hawaruhusiwi kuvaa nguo tofauti na hizo kiasi kwamba wakati wa baridi wanapata shidakubwa lakini hawana la kufanya.
“Hizi ndiyo nguo zetu rasmi hapa kazini. Tukivaa tofauti na hizi tunafukuzwa kazi, tunashukuru mmekuja wabunge wetu mtutetee tunaangamia,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.
Kwenye mgahawa wa wafanyakazi, hali pia ni mbaya na wabunge walishuhudia uchafu uliokithiri huku vyombo vya kulia chakula vikiwa vya plastiki jambo ambalo ni hatari kwa afya za wafanyakazi hao.
Baadhi ya wafanyakazi walisema licha ya kutumia vyombo vya plastiki pia wanalazimika kutumia vikombe kwa kupokezana kwa vile vilivyopo havitoshi.
“Hata sisi tunaonekana kana mbwa, angalieni sehemu hii tunayolia chakula. Haifai hata kwa mnyama mbwa maana ni chafu kupindukia lakini hawatujali,” walisema baadhi ya wafanyakazi.
Wafanyakazi wa kigeni
Mkurugenzi wa Kiwanda hicho, Manoj Suchak aliulizwa kuhusu hatua ya kuajiri wafanyakazi wa kigeni katika nafasi zote za juu bila kuhusisha mfanyakazi mzawa hata mmoja.
Akijibu swali hilo lililoulizwa na Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), alisema kati ya mameneja saba wa kiwanda hicho ni watano tu ambao ni wazawa.
Hata hivyo Nkamia alipotaka amwone angalau mmoja ambaye ni mzawa, alitokea kijana mwenye asili ya Asia, jambo lililozua kicheko na miguno kutoka kwa wabunge.
Ziara hiyo ya wabunge ilikuwa pamoja na mambo mengine kukagua mazingira ya kiwanda, kusikiliza mgogoro baina ya wafanyakazi na manejimenti ya kiwanda hicho ambao umedumu kwa muda mrefu.
* Wavutana katika kutembelea kiwanda
* Kiwandani wabunge washuhudia ‘madudu’
* Wafanyakazi wanalazimishwa kuvaa kaptura
* Wabunge watokwa machozi kwa waliyoyaona
Na Arodia Peter
Dar es Salaam
WAZIRI wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Gaudensia Kabaka jana alivutana vikali na wabunge wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii waliokuwa wanataka kutembelea Kiwanda cha Vyombo vya Nyumbani cha Jambo Plastiki kilichoko Dar es Salaam.
Wakati wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa wamekwisha kujiandaa kwenda katika kiwanda hicho jana, ghafla Waziri Kabaka aliwaeleza kuwa ziara hiyo imeahirishwa hadi wakati mwingine.
Kabaka alitoa sababu za kutaka kuahirisha ziara hiyo kuwa ni mgogoro wa wafanyakazi na mwajiri kiwandani hapo ambao upo mahakamani hivyo ziara hiyo itakuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Baada ya kutolewa taarifa hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jenista Mhagama alikuja juu na kumweleza Kabaka kuwa kamwe kamati yake haiwezi kuahirisha ziara hiyo bila kutolewa sababu za kuridhisha. Alisema kitendo alichokifanya Waziri kinadhalilisha kamati yake.
“Mheshimiwa Waziri kitendo ulichokifanya unaingiza mgogoro mkubwa katika kamati ya Bunge… kwa mazingira ya sasa Watanzania hawana mahali popote pa kutolea shida zao zaidi ya bunge na hii inadhihirika wazi wataalamu wako hawakukushauri vizuri,” alisema Mbunge huyo wa Peramiho kwa tiketi ya CCM na kuongeza:
“Basi kama ni hivyo, Mheshimiwa Waziri mimi nakupisha uwe mwenyekiti wa kamati ya Bunge maana naona hutaki kutuelewa.”
Kuona hivyo, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alikwenda mbali zaidi kwa kusema kwa uzoefu uliopo nchini unaonyesha kuwa ziara hiyo tayari imekwicha kuchakachuliwa na wahusika kwa manufaa wanayoyajua wao.
Alisisitiza kwamba kama ziara itaahirishwa basi yeye hatakuwamo kwenye orodha hiyo.
Naye Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) alisema kama kamati haitaki kwenda kwenye kiwanda hicho yeye atapanga ziara yake kama mbunge wa Chadema na kwenda kusikiliza na kukagua mazingira kiwandani hapo.
Asumpta Nshunju (CCM) ambaye ni Mbunge wa Nkenge, alisema kuna dalili za wazi watu wamepokea chochote kutoka kwa mwekezaji ndiyo maana kamati imepigwa ‘stop’ dakika za mwisho.
Akimsaidia waziri wake, Ofisa Kazi Mfawidhi wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Josephat Rugakingira aliwaambia wabunge kwamba haingekuwa vizuri kutembelea kiwanda hicho wakati mgogoro kati ya menejimenti na wafanyakazi bado uko Baraza la Usuluhishi wa Migogogro (CMA) ikiwa imefunguliwa kesi namba DMA/DSM/ILALA/ 2009.
Hata hivyo baada ya mvutano mkali hatimaye Waziri Kabaka alikubaliana na wabunge na kuamua kufanya ziara kiwandani hapo wakati huo ikiwa saa 7.00 mchana.
Kiwandani
Wabunge walipofika kiwandani walipangua ratiba iliyokuwa imeandaliwa iliyotaka wafanyakazi na menejimenti kukutana na kamati ya Bunge kwa pamoja.
Kamati ya Bunge iliamua kukutana na wafanyakazi pekee, kikao kilichodumu kwa zaidi ya saa moja. Waandishi wa habari wa menejimenti hawakuruhusiwa katika kikao hicho.
Baada ya kumalizika kikao hicho, wabunge walitoka nje wakiwa wanafuta machozi na baadhi yao walisema waliingiwa na simanzi kubwa kutokana na mambo mazito waliyoelezwa katika kikao hicho.
Hata hivyo, ilibainika kuwa katika kikao hicho ambacho Waziri pia alishiriki, kesi iliyokuwa inasemwa kuwa ipo mahakamani haikuwa kweli kwa vile ilikwisha kutolewa uamuzi tangu mwaka 2009.
“Hii kama siyo rushwa ni nini, ndiyo maana walitaka kutuchakachua tusije hapa kwa maslahi yao, hii ni aibu. Wataalamu wa Wizara ndiyo wanaotufanya sisi wabunge wa CCM tuonekane hatuna thamani mbele ya umma… kumbe ni watu wachache waliojiwekea mtandao wa rushwa kwa njia wanazozijua wao,” alisema mmoja wa wabunge kwa sharti la kutotajwa jina.
Waziri Kabaka akiri, aiomba radhi kamati
Baadaye Waziri Kabaka aliomba radhi kwa Kamati ya Bunge kutokana na hali iliyojitokeza awali. Alisema yeye hakujua kama alichoambiwa na wataalamu wa Wizara yake kilikuwa ni uongo na uzushi.
“Mheshimiwa mwenyekiti naomba radhi kwa yaliyotokea, nakiri nilidanganywa sasa nimejifunza kutoka kwenu,” alisema Kabaka kwa sauti ya upole.
Alipoulizwa na waandishi wa habari ni hatua gani atawachukulia wataalamu waliomdang’anya, alisema:
“Niachieni nitashughulika nao, tutaongea na wenzangu tuone ni kwa nini wamefanya hivyo”.
Wafanyakazi wanalazimishwa kuvaa kaptura
Kiwandani hapo wabunge walishuhudia wafanyakazi wakike na kiume wakiwa wamevaa kaptura na fulana ikiwa ndiyo sare za kiwanda hicho.
Wakizungumzia hali hiyo baadhi ya wafanyakazi walisema hawaruhusiwi kuvaa nguo tofauti na hizo kiasi kwamba wakati wa baridi wanapata shidakubwa lakini hawana la kufanya.
“Hizi ndiyo nguo zetu rasmi hapa kazini. Tukivaa tofauti na hizi tunafukuzwa kazi, tunashukuru mmekuja wabunge wetu mtutetee tunaangamia,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.
Kwenye mgahawa wa wafanyakazi, hali pia ni mbaya na wabunge walishuhudia uchafu uliokithiri huku vyombo vya kulia chakula vikiwa vya plastiki jambo ambalo ni hatari kwa afya za wafanyakazi hao.
Baadhi ya wafanyakazi walisema licha ya kutumia vyombo vya plastiki pia wanalazimika kutumia vikombe kwa kupokezana kwa vile vilivyopo havitoshi.
“Hata sisi tunaonekana kana mbwa, angalieni sehemu hii tunayolia chakula. Haifai hata kwa mnyama mbwa maana ni chafu kupindukia lakini hawatujali,” walisema baadhi ya wafanyakazi.
Wafanyakazi wa kigeni
Mkurugenzi wa Kiwanda hicho, Manoj Suchak aliulizwa kuhusu hatua ya kuajiri wafanyakazi wa kigeni katika nafasi zote za juu bila kuhusisha mfanyakazi mzawa hata mmoja.
Akijibu swali hilo lililoulizwa na Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), alisema kati ya mameneja saba wa kiwanda hicho ni watano tu ambao ni wazawa.
Hata hivyo Nkamia alipotaka amwone angalau mmoja ambaye ni mzawa, alitokea kijana mwenye asili ya Asia, jambo lililozua kicheko na miguno kutoka kwa wabunge.
Ziara hiyo ya wabunge ilikuwa pamoja na mambo mengine kukagua mazingira ya kiwanda, kusikiliza mgogoro baina ya wafanyakazi na manejimenti ya kiwanda hicho ambao umedumu kwa muda mrefu.
Wednesday, May 11, 2011
Mama wa mtoto mwenye matatizo ya kutokuwa na sehemu ya kutolea haja kubwa akipokea msaada wa Tshs 600,000/= kutoka kwa Mh Joseph O Mbilinyi Mbunge wa Mbeya mjini ili aweze kumpeleka Hospitali ya Peramiho kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji kwa mujibu wa gharama hiyo ambayo Mama huyo alielezwa ikipatikana ndio ataweza kufanyiwa upasuaji. Mungu atamsaidia atapona!
Mama wa mtoto mwenye matatizo ya kutokuwa na haja kubwa akitoa maelezo ya mtoto wake mwenye umri wa miaka 2 kwa waandishi wa habari na Mh Mbunge wa Mbeya mjini ambaye aliguswa na tatizo la mtoto huyo na kuamua kumsaidia..
Mh Mbunge wa Mbeya mjini akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa NIMR na baadhi ya maafisa waandamizi wa kituo hiko alipotembelea katika moja ya shughuli zake anazozifanya jimboni kwake.
Mh Joseph O Mbilinyi Mbunge wa Mbeya mjini akiwa katika moja ya zira anazoendelea kuzifanya na hapa akiwa katika uwanja unaoendelea kujengwa wa Songwe International Airport uliopo Songwe-Mbeya. Katika picha anaonekana akipewa maelezo na Meneja mradi huku wakiwa wamesimama eneo la runaway ambalo tayari km 2 zimewekwa lami na ujenzi bado unaendelea......kwa maelezo ya meneja mradi kufikia mwezi wa 8 tayari uwanja utakuwa umekamilika na kazi inayobaki ni kwa serikali kukamilisha taratibu za ofisi na mambo mengineyo.
Mh Joseph O Mbilinyi Mbunge wa Mbeya mjini akiwa katika ziara ya kituo cha utafiti cha NIMR kilichopo Mbeya mjini ndani ya Hospitali ya rufaa,kama anavyoonekana akipata maelezo kutoka kwa Managing dector wa MMRP Mr Leonard Maboko. Baada ya hapo alitembelea maabara zote zilizopo kituoni hapo na kujionea shughuli za utafiti pamoja na kupata maelezo ya kina kuhusiana na shughuli zinazofanywa na kituo hiko
Mh Joseph O Mbilinyi{MP} akiwa katika moja ya ziara zake jimboni Mbeya,hapa alikuwa ametembelea MBEYA DRY PORT na kujionea mazingira yake pamoja na kujadiliana na uongozi kujua ni kwa nini kituo hakifanyi kazi kwani ni moja kati ya sehemu ambayo ingeweza kutoa ajira zaidi ya 300. Kulia ni mkurugenzi wa kituo hiko na kushoto kwa Mbunge ni Fuel Depot manager Mr Suleiman Issa Soloka,akifuatiwa na Mrs Tabu Kaihula......hapa wakiangalia na kuteta jambo juu ya crane ya kunyanyulia containers.
Mkutano uliofanyika Uyole-Kibonde nyasi,Mh Joseph O Mbilinyi akiwashukuru wananchi na pia kuwafafanulia baadhi ya mambo jimboni kwake...hiii ni baada ya kutoka bungeni Dodoma.
Friday, May 6, 2011
CHADEMA WAMSHAMBULIA PROF. MWANDOSYA
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Mr II Sugu, amemtaka Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Prof. Mark Mwandosya, kutumia muda wake wa uongozi uliosalia kwa ajili ya kujiandaa na kustaafu kwa kuwa ndoto zake za kutaka urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haziwezi kutimia.
Pia alisema ni vigumu tena kwake kuendelea kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki.
Sugu aliyasema hayo wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa ‘Chadema Twanga Kotekote’ ulofanyika katika kijiji cha Kandete, eneo la Mwakaleli Jimbo la Rungwe Mashariki ambalo hivi sasa linashikiliwa na Prof. Mwandosya.
Mkutano huo ni moja ya mikutano mingi itakayoendelea kufanyika katika jimbo hilo, ambayo imepewa jina la ‘Operesheni Giant Ndosya, yenye lengo la maandalizi ya kumg’oa Prof. Mwandosya katika jimbo hilo kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Sugu alisema Prof. Mwandosya hajalitendea haki jimbo lake kwa kuwa wananchi hao wamempa ridhaa ya kuwaongoza kwa zaidi ya miaka 15, tena akiwa na wadhifa mkubwa serikalini, lakini kwa muda wote huo ameshindwa kuwajengea wananchi wake barabara kuanzia Katumba hadi Mwakaleli yenye urefu wa kilometa 30 tu.
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi Joseph Mbilinyi (SUGU) akiwa jukwaani kwenye moja ya mikutano
Alisema hata kama Prof. Mwandosya akichaguliwa kuwa rais hatawakumbuka wananchi wa Rungwe na badala yake atafanyia sherehe za kujipongeza Dar es Salaam, kwa kuwa huku kwao hakuna barabara alizojenga anazoweza kupitisha magari ya Ikulu.
Aidha Sugu alisema anamshangaa Prof. Mandosya kutotumia elimu kubwa aliyonayo kusoma alama za nyakati na kuendeleza fikra za kutaka urais akiwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho Sugu alidai kuwa kuna kila dalili kwamba kufikia mwaka 2015 chama hicho kinaweza kisiwepo.
“Nawaomba siku akija hapa mpeni ujumbe huu kuwa ajiandae kustaafu kwa kuwa hakuna urais wala ubunge tena kwake, namshauri arudi kufundisha darasani kwa kuwa hilo ndilo bado tunalihitaji kutoka kwake,” alisema Sugu huku akishangiliwa.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Eddo Mwamalala, alisema mikutano ya Twanga Kotekote wilayani Rungwe ambayo imeongezewa jina la ‘Operesheni Giant Ndosya’ inalenga kung’oa meno ya Mwandosya ya utawala wake wa kiimla katika Jimbo la Rungwe Mashariki.
Mwamalala alisema Mwandosya amewalemaza wakazi wa Rungwe Mashariki kimaendeleo na kuwa katika hilo hawawezi kumwonea huruma, hivyo akawataka wananchi wa Rungwe Mashariki kuunga mkono harakati hizo za ukombozi wao.
“Hakuna kumwonea huruma Mwandosya kwa kuwa ametulemaza kimaendeleo, hata hawa madiwani wabovu mliowachagua mmewachagua kwa jina la Mwandosya, kubwa tunalowaombeni wananchi wa Rungwe ni kutuunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa jimbo hili,” alisema Mwamalala.
Kiongozi wa kikosikazi cha Chadema Twanga Kotekote, John Mwambigija, alisema Mwandosya badala ya kufikiria maendeleo ya jimbo lake ameanza kampeni chafu ya kuwarubuni na kuwanunua viongozi wa Chadema na kuwaingiza CCM.
Alidai kuwa kwa kitendo hicho cha Mwandosya ajue kuwa jimboni kwake hayuko salama. Alisema Mwandosya asahau tena ubunge mwaka 2015 na kama anahitaji kupona akimbilie kugombea urais.
Timu hiyo ya Kikosikazi Chadema Twanga kotekote leo inahamia mjini Tukuyu katika jimbo linaloongozwa na aliyekuwa Waziri wa Afya, Prof. David Mwakyusa, kwa ajili ya kuendeleza harakati zake za kukijenga chama.
Baada ya mkutano huo, Chadema Twanga Kotekote itasitisha mikutano yake ili kupisha maandalizi ya maandamano ya kitaifa ya Operesheni Sangara ambayo yanatarajiwa kufanyika Mei 4, mwaka huu jijini Mbeya.
Saturday, April 9, 2011
Studio ya JK yazua mjadala bungeni
| ||
|
Wednesday, April 6, 2011
Mbunge Joseph Mbilinyi apinga kiwanda kugeuzwa ghala la bia.
Na Joachim
Nyambo,Mbeya
MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Mr II, amesema
kitendo cha serikali mkoani hapa kukabidhi majengo ya kilichokuwa
kiwanda cha zana za kilimo (ZZK) yaliyopo eneo la Iyunga jijini hapa
kwa kampuni ya vinywaji ya TBL yatumike kama maghala kinakinzana na
mpango wa serikali wa kufufua viwanda muhimu kama hicho.
Mhe. Joseph Mbilinyi (Sugu) akiwa katika moja ya mikutano yake
Kabla ya kusimamisha uzalishaji wa zana zaidi ya miaka kumi iliyopita
hali iliyosababishwa na mwekezaji aliyekabidhiwa kushindwa kukiendesha
kiwanda hicho kilikuwa tegemeo kubwa la wananchi wa mkoa wa Mbeya
ambao asilimia yao kubwea ni wakulima.
Akizungumza na mamia ya wakazi wa kata za Nsalaga na Uyole katika
viwanja vya kibonde Nyasi, Mbunge huyo amesema hatua hiyo moja kwa
moja imewapa hofu wananchi kuwa huenda serikali haina mpango tena wa
kukifufua ili kiendelee na uzalishaji wa zana hizo ambao utaweza
kuwapunguzuia gharama za ununuzi wa pembejeo tofauti na ilivyo hivi
sasa.
Amesema inashangaza kuona kuwa baadhi ya watendaji wa serikali ambayo
kila siku inahubiri mpango wa kukuza uchumi wa wananchi wake kupitia
kilimo kwa sera mbalimbali ikiwemo Kilimo Kwanza wanakubali kumpa
mwekezaji ambaye anayegeuza kiwanda cha ZZK kuwa ghala la kuhifadhia
bia.
Amesema wananchi wa mkoa wa Mbeya kwa ujumla walikitegemea sana
kiwanda hicho kiweze kufufuliwa na kuzalisha zana za kilimo ambazo
zingepatikana kwa urahisi kwani zingeuzwa kwa bei ndogo kwa wakulima
ili waweze kuboresha kilimo chao lakini sasa matumaini yao yameanza
kufifia.
Mbilinyi amesema kama kiwanda hicho kingefufuliwa hata Trekta ndogo
aina ya Powertiller zinazoagizwa nje ya nchi kwa bei kubwa zingeweza
kuzalishwa katika kiwanda hicho na kuuzwa kwa bei ambayo wakulima
wangemudu kununua.
Hata hivyo Mbilinyi amesema yupo tayari kubisha hodi katika ofizi za
Waziri wa Viwanda ili apewe maelezo ya kina juu ya mwongozo uliotumika
kwa serikali kugeuza kiwanda hicho kuwa ghala la kuhifadhia bia badala
ya kuweka mikakati ya kukifufua.
Aidha Mbunge huyo amepongeza hatua ya seriakali kujenga uwanja wa
ndege wa Songwe , akisema ameridhishwa hatua za ujenzi zinazoendelea
baada ya kuutembelea na kuelezwa na wataalamu kuwa ifikapo Agosti
mwaka huu ndege zitakuwa zimeanza kutua katika uwanja huo.
Mbilinyi amesema kukamilika kwa uwanja huo ni changamoto kubwa ya
maendeleo katika mkoa wa Mbeya na kuwataka wananchi kujiandaa vyema
kuutumia uwanja huo kwa manufaa hususani kwa kuzalisha mazao
yanayoweza kusafirishwa nje ya nchi na kuuzwa kwa bei yenye kuwaletea
tija.
Siku Mhe. Joseph Mbilinyi Alipotembelea Jukwaa La Sanaa
Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi maarufu kwa Jina la Sugu akiongea na wadau wa Jukwaa la Sanaa jana wakati alipohudhuria kwa mara ya kwanza toka achaguliwe kuwa mbunge. Sugu ni moja ya wadau wa Jukwaa hilo linalofanyika kila Jumatatu Ukumbi wa BASATA.Profesa Amandina Lihamba kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akichokoza mada kuhusu tasnia ya Filamu hapa nchini kwenye Jukwaa la Sanaa BASATA jana. Kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego.
Na Mwandishi Wetu:
Jukwaa la Sanaa BASATA limempongeza kwa ushindi wa ubunge na kumpa kazi ya kutetea maslahi ya wasanii Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye pia ni mmoja wa waasisi wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina Sugu.
Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye ukumbi wa BASATA kwa niaba ya wadau wote. Profesa Amandina Lihamba kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye alikuwa ni Mratibu wa Jukwaa hilo alisema kwamba, wadau wa Jukwaa la Sanaa wanampongeza kwa dhati kwa ushindi wake na wanamtuma bungeni kutetea haki zao na kwamba asiwatupe.
“Tunajua toka ushinde leo ni mara yako ya kwanza kuonana na hadhira ya wasanii hivyo tunachukua fursa hii kukupongeza kwa dhati, uendelee na moyo huo huo wa kuwapigania wasanii na usiwatupe” aliongeza Profesa Lihamba.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego alisema kwamba, pamoja na BASATA awali kutuma barua ya pongezi kwake na kwa wabunge wengine wasanii, bado Jukwaa la Sanaa lina kila sababu ya kumpongeza na kumtuma kwenda kutetea haki za wasanii na kuhakikisha maslahi ya sekta ya sanaa yanalindwa.
“Naomba niungane na wenzangu kutambua uwepo wa Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini, msanii mwenzetu naimani sasa tunapozungumza hapa katika Jukwaa tunazungumza na mtu ambaye sasa atakuwa bungeni akiwakilisha wasanii. Pamoja na barua ya kumpongeza tuliyomtumia yeye na wasanii wengine walioingia bungeni, tunampongeza tena kwa dhati” alisema Materego.
Naye Mbilinyi aliyeambatana na Katibu wake Fred Maliki, maarufu kwa jina la usanii la Mkoloni alimshukuru Materego kwa pongezi zake lakini akapongeza juhudi anazochukua katika kuwahabarisha na kuwapa fursa ya elimu wadau wa sanaa. Aliahidi kuendeleza harakati za kupigania haki za wasanii kwani ndicho kitu ambacho ataanza nacho.
“Harakati za kupigania haki za wasanii nimezianza kwa muda mrefu nawaahidi kwamba sitarudi nyuma na kwa sasa napenda niwaambie kwamba, mapambano ndiyo kwanza yameanza kwani sasa ndiyo tumekabidhiwa rungu” alimalizia Mbilinyi ambaye aliwahi kutamba na nyimbo kama za Mikononi mwa polisi, Deiwaka, Dar moto chini, Wananiita Sugu, Hold On na nyingine nyingi.
Jukwaa la Sanaa BASATA limempongeza kwa ushindi wa ubunge na kumpa kazi ya kutetea maslahi ya wasanii Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye pia ni mmoja wa waasisi wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina Sugu.
Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye ukumbi wa BASATA kwa niaba ya wadau wote. Profesa Amandina Lihamba kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye alikuwa ni Mratibu wa Jukwaa hilo alisema kwamba, wadau wa Jukwaa la Sanaa wanampongeza kwa dhati kwa ushindi wake na wanamtuma bungeni kutetea haki zao na kwamba asiwatupe.
“Tunajua toka ushinde leo ni mara yako ya kwanza kuonana na hadhira ya wasanii hivyo tunachukua fursa hii kukupongeza kwa dhati, uendelee na moyo huo huo wa kuwapigania wasanii na usiwatupe” aliongeza Profesa Lihamba.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego alisema kwamba, pamoja na BASATA awali kutuma barua ya pongezi kwake na kwa wabunge wengine wasanii, bado Jukwaa la Sanaa lina kila sababu ya kumpongeza na kumtuma kwenda kutetea haki za wasanii na kuhakikisha maslahi ya sekta ya sanaa yanalindwa.
“Naomba niungane na wenzangu kutambua uwepo wa Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini, msanii mwenzetu naimani sasa tunapozungumza hapa katika Jukwaa tunazungumza na mtu ambaye sasa atakuwa bungeni akiwakilisha wasanii. Pamoja na barua ya kumpongeza tuliyomtumia yeye na wasanii wengine walioingia bungeni, tunampongeza tena kwa dhati” alisema Materego.
Naye Mbilinyi aliyeambatana na Katibu wake Fred Maliki, maarufu kwa jina la usanii la Mkoloni alimshukuru Materego kwa pongezi zake lakini akapongeza juhudi anazochukua katika kuwahabarisha na kuwapa fursa ya elimu wadau wa sanaa. Aliahidi kuendeleza harakati za kupigania haki za wasanii kwani ndicho kitu ambacho ataanza nacho.
“Harakati za kupigania haki za wasanii nimezianza kwa muda mrefu nawaahidi kwamba sitarudi nyuma na kwa sasa napenda niwaambie kwamba, mapambano ndiyo kwanza yameanza kwani sasa ndiyo tumekabidhiwa rungu” alimalizia Mbilinyi ambaye aliwahi kutamba na nyimbo kama za Mikononi mwa polisi, Deiwaka, Dar moto chini, Wananiita Sugu, Hold On na nyingine nyingi.
Mr II ajisifu kwa kuweka historia bungeni
MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Mr II au Sugu’ ametamba na kujifafanisha na Spika wa Bunge, Anne Makinda katika kuweka historia ya yeye kuwa msanii wa kwanza wa muziki wa bongo flava kuingia bungeni kama ilivyo kwa Spika ambaye ni mwanamke wa kwanza kuongoza Bunge.
Mbilinyi, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alitoa majigambo hayo jana wakati akisoma maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Azimio la Serikali la Kuridhia Mkataba wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) la Kulinda Urithi wa Utamaduni Usioshikika wa mwaka 2003.
Azimio hilo liliwasilishwa jana bungeni na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi. Kabla ya kutoa maoni hayo, Mbilinyi alisema, “Kwa heshima kubwa niwashukuru wananchi wa Mbeya Mjini kuniwezesha kuweka historia ya kuwa msanii wa kwanza wa Bongo Flava kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mheshimiwa Spika, mimi na wewe tumeingia katika historia kupitia Bunge hili la kumi, kwa mimi kuwa msanii wa kwanza wa Bongo Flava kuingia bungeni na wewe kuwa Spika wa kwanza mwanamke kuliongoza Bunge,” alisema Mbilinyi na kufanya wabunge kuangua kicheko.
Mbilinyi baada ya kueleza kuwa suala hilo ni la kihistoria na yeye anafarijika ameingia katika historia, alimpongeza Makinda na kuendelea kutoa maoni ya kambi ya upinzani yaliyounga mkono hoja hiyo na kueleza kuwa azimio linalenga kulinda hadhi ya Mtanzania.
Baada ya maoni ya Kambi hiyo ya Upinzani, baadhi ya Wabunge walipata fursa ya kuchangia azimio akiwemo msanii mwingine, Mbunge wa Viti Maalum, Vick Kamata (CCM) ambaye aliunga mkono hoja na kueleza kuwa mkataba huo ukiridhiwa utawawezesha wasanii kutambulika kimataifa na kazi zao kuweza kulindwa kwa kuwa suala la hatimiliki limezingatiwa kwa upana katika mkataba huo.
Mbilinyi, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alitoa majigambo hayo jana wakati akisoma maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Azimio la Serikali la Kuridhia Mkataba wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) la Kulinda Urithi wa Utamaduni Usioshikika wa mwaka 2003.
Mh Joseph Mbilinyi a.k.a Mr II akipongezwa na Spika wa Bunge Mh Anna Makinda
Azimio hilo liliwasilishwa jana bungeni na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi. Kabla ya kutoa maoni hayo, Mbilinyi alisema, “Kwa heshima kubwa niwashukuru wananchi wa Mbeya Mjini kuniwezesha kuweka historia ya kuwa msanii wa kwanza wa Bongo Flava kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mheshimiwa Spika, mimi na wewe tumeingia katika historia kupitia Bunge hili la kumi, kwa mimi kuwa msanii wa kwanza wa Bongo Flava kuingia bungeni na wewe kuwa Spika wa kwanza mwanamke kuliongoza Bunge,” alisema Mbilinyi na kufanya wabunge kuangua kicheko.
Mbilinyi baada ya kueleza kuwa suala hilo ni la kihistoria na yeye anafarijika ameingia katika historia, alimpongeza Makinda na kuendelea kutoa maoni ya kambi ya upinzani yaliyounga mkono hoja hiyo na kueleza kuwa azimio linalenga kulinda hadhi ya Mtanzania.
Baada ya maoni ya Kambi hiyo ya Upinzani, baadhi ya Wabunge walipata fursa ya kuchangia azimio akiwemo msanii mwingine, Mbunge wa Viti Maalum, Vick Kamata (CCM) ambaye aliunga mkono hoja na kueleza kuwa mkataba huo ukiridhiwa utawawezesha wasanii kutambulika kimataifa na kazi zao kuweza kulindwa kwa kuwa suala la hatimiliki limezingatiwa kwa upana katika mkataba huo.
Naye Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama (CCM) alisema kilio cha wasanii wa nyimbo za asili zinazobeba utamaduni wa Kitanzania, kimefika mahali pake na kutaka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, kupigwe nyimbo za asili za makabila yetu badala ya nyimbo za kigeni zinazopigwa hivi sasa.
Monday, March 28, 2011
Saturday, March 12, 2011
mkutano wa kujadili maendeleo Uyole-kibonde nyasi
Mh Joseph O Mbilinyi mbunge wa Mbeya mjini akiwahutubia wananchi wa jimbo la Mbeya mjini katika eneo la Kibonde nyasi Uyole jijini Mbeya pamoja na kuwashukuru pia alikuwa akitumia fursa hiyo kuchukua maswali mbali mbali kwa wananchi kabla ya kwenda Bungeni tarehe 5-4-2011.
Thursday, December 30, 2010
SUGU NA MAISHA YA KILA SIKU KAMA MBUNGE
Mh SUGU akifanya kazi ofisini kwa kwake
Bwana Daniel Kamili ( Danny Msimamo ) akiwa katika meza ya mapokezi tayari kwa kuwa hudumia Wanambeya
Katibu wa Mbunge ( Mkoloni ) pamoja na Sugu nyumbani wakibadilishana mawili matatu mara baada ya kutoka ofisini
Hapa Danny msimamo akibadilishana mawili matatu na Mh SUGU
Sugu akiwa nyumbani kwake
Subscribe to:
Posts (Atom)










