Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Sunday, September 23, 2012

Thursday, September 20, 2012

MBUNGE "SUGU" ATEMBELEA SWAGGA FIJHO ARTS CENTRE

Mbunge Joseph Mbilinyi SUGU mwenye miwani akiwa na baadhi ya Wasanii wanaopata mafunzo katika kituo Cha SWAGGA FIJHO ARTS CENTRE jijini Mbeya kulia kwake ni mdau Kwame Elly Anangisye

MBEYA KUELEKEA KUWA JIJI KAMILI... UJENZI WA BARABARA ZA KIWANGO CHA LAMI UNAENDELEA KILA KONA YA JIJI...





TUKO BIZE JIMBONI..... JIJINI MBEYA NI KIKAZI ZAIDI!

 Soko jipya la Mwanjelwa ambalo linaendelea kujengwa kama linavyoonekana ambalo likikamilika linategemea kuwa kitovu cha biashara cha nchi za kusini mwa Afrika
 CENTURY PLAZA - Mwanjelwa Mbeya
 Hapa ndio Kabwe....... ulipoanzia mtiti wa Machinga na kumalizikia..
Moja ya Mabanda ya Wamachinga yanayojengwa pembezoni mwa soko la Mwanjelwa na standa ya Kabwe..... Ahsante Halmashauri ya jiji la Mbeya kwa kuyafanyia kazi mawazo ya Mbunge

R.I.P. BRO YOHANA MWAKATOBE, MBUNGE ALIPOKUWA MSIBANI

Jiji la Mbeya lilikumbwa na simanzi pale alipofariki mmoja wa kijana maarufu Yohana Mwakatobe ambaye alikuwa anapatikana haswa mitaa ya Mwanjelwa na Mafiat, Mazishi yalifanyika nyumbani kwao Mwanjelwa Mbeya na baadaye kuzikwa kwenye makaburi ya Sabasaba
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI!
 Hapa Mbunge Joseph Mbilinyi akiwa na baadhi ya waombolezaji msibani
 Mheshimiwa SUGU akiongea neno kwa waombolezaji msibani
Hapa ni makaburini Mbunge akiwa na viongozi wa CHADEMA -jijini Mbeya
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Mtaa CHADEMA, Katibu wa CHADEMA Mbeya mjini Criss Mwamsiku, Diwani viti maalumu CHADEMA wakimkaribisha Mbunge alipowasili msibani

Friday, May 18, 2012

KATIKA MUENDELEZO WA ZIARA ZA MH. SUGU, MIKUTANO YA LEO KATA ZA MABATINI NA ITENDE.....KILINUKA KAMA KAWA


Mbeyaaaa!!!!!! ooooooooooooyeeeeeee !!!!! watu " oooyeeeeeeeeeee"

Mzuka wa Chadema na Mbunge wao ukiwa umepanda kwani Mbeya, Mh Sugu hufaha mika kama Raisi wa Mbeya .


Mbunge wa Mbeya Mjini akiwapa ripoti ya kazi Wanambeya juu ya ninikina endelea katika maendeleo ya jiji lao


Takataka haikuwa tatizo kwani watu wanahamu ya kumsikiliza Mbunge wao kiasi cha kukaa ndani na juu ya Ghuba la taka


Umakini mkubwa ulitapakaa kwa Wanambeya wakimsikiliza Mh Sugu kwa makini 

Wazee nao hawako nyuma kwenye mabadiliko ya nchi haswa kwenye mambo muhimu ya jiji la Mbeya kwani wamekuwa bega kwa bega na Mbuge wao

Mbuge akiweka mkazo katika suala la sensa mwaka 2012 kwa wana wa Itende

Mh Mbilinyi alipata nafasi ya kutembelea ofisi ya afisa mtendaji pia ilikupata taarifa na matatizo yanayo wakabili watendaji wa kata kulia kwake ni Mwenyekiti Chadema Mbeya Mjini Bwana John Mwambigija  .

Katibu wa Chadema Mbeya Mjini Bwana Criss Mwamsiku kushoto na Mh Sugu baada ya kusaini kitabu cha wageni katika ofisi ya kata ya Chadema Itende

Mh sugu akipata chakula chamchana katika ofisi ya Chadema kata ya Itende huku akiwatia moyo nakuwapa ujasili wana itende kwa kazi nzuri ya ujenzi wa ofisi hiyo ya chama .

Thursday, May 17, 2012

MH. JOSEPH MBILINYI (SUGU) AENDELEA NA ZIARA YAKE KATIKA JIMBO LA MBEYA MJINI

 Mbunge wa Mbeya Mjini akipokelewa na wananchi wa Kata ya Nsoho kabla ya kufanya mkutano mkubwa wa hadhara katika eneo hilo lililo nje kidogo ya mji wa Mbeya 
 Hapa  Mbunge wa Mbeya mjini akiwaelezea wananchi wa kata ya Iziwa baadhi ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo zilizofanyika mpaka sasa hapa Jimboni
 Wananchi wakimsikiliza kwa makini Mh. Joseph Mbilinyi (Sugu) alipokuwa akiwahutubia wananchi katika ziara ya jimboni kwake Mbeya mjini

 Sugu akisisitiza jambo kwa wananchi wa kata ya Iziwa wakati wa ziara yake ya kuzungukia kata zote za jimbo la Mbeya Mjini
 Wananchi waki msikiliza Mbunge wao Joseph Mbilinyi (Sugu) wakati akiwahutubia katika kiwanja cha kilabu cha Iziwa 
 Mheshimiwa Sugu akikazia jambo ambalo Kamanda Kwame Elly Anangisye (pichani) alikuwa akilipigania kwa maendeleo ya wakazi wa jiji la Mbeya
 Watu wa rika tofauti wa Kata ya Iziwa  wakimsikiliza Mbunge wao Joseph Mbilinyi
  
Mh. Mbilinyi akisikiliza swali lililoandaliwa na Wananchi ili akaulize kwa niaba yao kwenye vikao vijavyo vya Bunge la bajeti.

Tuesday, May 15, 2012

MBUNGE WA MBEYA MJINI JOSEPH MBILINYI (SUGU) AANZA ZIARA YA KUZUNGUKA JIMBONI

    Wananchi wa kata wa Ituha wakimsikiliza kwa makini Mbunge wao Joseph Mbilinyi (Sugu)

 Mbunge wa Mbeya mjini akielezea shughuli za utekelezaji ahadi zilizofanyika mpaka kufikia kipindi hiki
 Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, Katibu CHADEMA wilaya Criss Mwamasiku (kushoto) na Kamanda Kwame Elly Anangisye (nyuma) wakisikiliza kero na maoni ya wananchi wa kata ya Ituha
 Mwananchi wa Kata ya Ituha akitoa malalamiko yake mbele ya Mbunge wa Mbeya mjini
Wananchi wa Kata ya Ituha wakimsikiliza Mbunge wao Joseph Mbilinyi (Sugu) katika ziara yake ya kutembelea kata za Mbeya mjini