Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Monday, August 23, 2010

Kwa nini nimeanzisha Blog?

Mimi ni Joseph Mbilinyi aka SUGU, Mr II, au zamani 2 Proud. Ni ndugu yenu na mwenzenu.
Nimeanzisha Blog ili kupata maoni na mapendekezo mbalimbali katika mapambano yangu. Nilikuwa mwanaharakati kwa muda mrefu kupitia muziki na sasa nimeamua kuendeleza harakati kwa style nyingine ya siasa maana wanasema "aliye juu mngoje chini" na nimesubiri sana chini lakini nikaona ni bora niende hukohuko juu na labda nitasikilizwa.
Nimeanzisha Blog ili nipate ushirikiano kwa ndugu zangu toka pande zoote za dunia ili tusaidiane kuiendeleza Mbeya na Tanzania yetu kwa ujumla ambayo inatuhitaji sisi, ningependa sana vijana tuchangamke na kupambana ili Tanzania yetu ikae sawa na tuendelee katika kila nyanja ya kipato, kielimu na kiafya na mambo mengine.
Naomba ushirikiano wenu ndugu zangu.

No comments:

Post a Comment